Polisi Na Majambazi Wakabiliana Vikali, Muthangari
У вашего броузера проблема в совместимости с HTML5
Afisa mkuu wa polisi anayesimamia kituo cha polisi cha Muthangari Krop Lipa amejeruhiwa vibaya, baada ya kupigwa risasi tumboni na majambazi katika eneo la Lavington. Lipa, ambaye tayari amefanyiwa upasuaji alijeruhiwa kwenye makabiliano ambayo yalipelekea kikosi cha maafisa wa Recce kupelekwa katika eneo hilo na kukabiliana na majambazi hao. Hii hapa taarifa ya patashika iliyofuatia kati ya maafisa hao wa kikosi cha Recce na majambazi hao.